Ndugu wa marehemu watano waliofariki katika ajali Kibiti watakiwa kufika Muhimbili kufanyiwa DNA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) imepokea maiti tano za ajali ya gari iliyotokea Kibiti mkoani Pwani ili kufanyiwa vina saba (DNA).

Miili hiyo ni ya watu wazima wanne na mtoto mmoja imeungua sana (beyond recognition) kwamba utambuzi wake ni mgumu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma,
Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminieli Aligaesha, alieleza kuwa tayari Hospitali ya Taifa Muhimbili imefanya uchunguzi (postmortem) na kuchukua sampuli kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha Forensic Pathology pamoja na Mkemia Mkuu wa Serikali ili kufanya uchunguzi zaidi.

“Tunawaomba ndugu wa karibu wa marehemu hawa hususani baba, mama na watoto kujitokeza kuanzia kesho tarehe 2 Septemba, 2019 saa mbili asubuhi ili kuchukuliwa sampuli na Mkemia Mkuu wa Serikali ili kusaidia kufanya uchunguzi wa kulinganisha vinasaba kati ya ndugu na marehemu na ili waweze kupewa miili hiyo kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi kukamilika,” alieleza

Miili ya marehemu watano walifariki kwenye ajali ya lori la Dangote lililogongana na gari ndogo kisha kuwaka moto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji, Onesmo Lyanga amesema miili ya watu watatu waliokuwa kwenye Lori la Dangote haijaweza kutambulika mara moja kutokana na kuteketea kwa moto.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad