Hakimu ‘Akwama’ Kesi ya Kabendera

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KESI ya Uhujumu uchumi inayomkabili mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Erick Kabendera, imeshindwa kuendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na Hakimu anayesikiliza kesi hiyo kutokuwepo mahakamani.



Kesi hiyo imetajwa na kuahirishwa mahakamani hapo mbele Hakimu Mkazi Vick Mwaikambo. Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon amedai mbele ya Hakimu Mwaikambo, kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.



Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mwaikambo ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 7, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashitaka matatu likiwemo la utakatishaji wa zaidi ya sh Milioni 173.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad