Ray C Amiss Maisha ya Skendo...Aonesha Msambwanda Wake Live

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





WAKATI Bongo watu wakimisi picha za utupu za mastaa kutokana na sheria ya makosa ya mtandao kung’ata wengi, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amejilipua huko majuu.  Ray C ambaye ni msanii maarufu anayeishi nchini Uingereza kwa sasa, ametupia hivi karibuni picha tata kwenye ukurasa wa Instagram na kuzua gumzo.

“Naona umemisi maisha ya skendo, unajitoa fahamu eee,” komenti ya dada mmoja ilisomeka kwenye ukurasa aliotumia staa huyo wa kitambo kuweka picha hiyo ya nusu utupu. Jicho la mwandishi wetu limeiona picha hiyo aliyoiweka mtandaoni akionekana amekaa kitandani huku akiwa amevaa kinguo kilichoacha sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa wazi.

Mbali na kinguo kuacha sehemu kubwa wazi, lakini pia kilikuwa na matundumatundu ambapo wengi walipoiona walisema: “Angekuwa Bongo staa huyo angeuona mkono wa serikali.” Aidha, Ray C hakuonekana kujali komenti za waliokosoa picha hiyo, hata mwandishi wetu alipomtafuta kupitia mawasiliano ya meseji ya WhatsApp kujua kilichomchachua hadi kuweka picha hiyo mtandaoni, hakujibu.

Ray C amepita katika maisha ya ustaa kutokana na kazi yake ya sanaa kabla ya kutopea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya, kisha kuachana nayo na kutimkia majuu kula bata. Mara kadhaa ameonekana akiwa krozi na mwanaume wa Kizungu ambaye anatajwa kuwa mchumba wake na kwamba ndiye anayempa jeuri ya maisha kwa sasa

SOMA HABARI HIZI KIRAHISI KUPITIA APP YETU YA UDAKU SPECIAL DOWNLOAD HAPA
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad