Trump asaini agizo la Rais kudhibiti mitando ya kijamii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais wa Marekani Donald Trump ameamua kuweka saini ya kuondoa baadhi ya marufuku ya kisheria ambayo mitandao ya kijamii inayo.

Saini hiyo inampa mamlaka ya kuweka hatua za kisheria dhidi ya makampuni ya mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter katika sheria walizoweka katika maudhui wanayochapisha katika mitandao yao.

Rais Trump ameishutumu mitandao ya kijamii kwa kushindwa kuwa makini wakati wa kusaini mamlaka ambayo iko huru kuondolewa wakati wa kuweka saini.

Amri hiyo inatarajiwa kukabiliwa na changamoto za kisheria.

Wataalamu wa kisheria wanasema kuwa bunge la Marekani au mfumo wa mahakama lazima iusike ili kubadili sheria iliyopo sasa ambayo inaeleweka kuwa inalinda mitandao ya kijamii.

Bwana Trump amekuwa akiishutumu mitandao ya kijamii kila mara kuharihi sauti yake au hat ahata kuweka sauti ambayo hajazungumza lakini anakuwa anasikika kama yeye.

Jumatano, bwana Trump aliishutumu Twitter kwa kuingilia uchaguzi baada ya kuongeza maelezo ya tweet mbili kama uthibitisho.

Alhamisi , Twitter iliongeza taarifa za kuhakiki taarifa kuhusu Covid-19" na kujumuisha ujumbe wa tweet kutoka kwa msemaji wa serikali ya China anayedai kuwa virusi vya corona vilitengenezwa Marekani.

Amri hiyo inasemaje?
Amri hiyo imewekwa ili kufafanua sheria ya mawasiliano ya staha ambayo Marekani imeweka katika mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na Youtube pamoja na ulinzi wa kisheria katika hali fulani.

Chini ya kifungu cha sheria cha namba 230, mitandao ya kijamii haiwajibishwi kwa maudhui ambayo watumiaji wake wanaweka mtandaoni lakini inaweza kuhusika kwa upande wa usamaria mwema wa kuondoa maudhui hayo mtandaoni ambayo labda yana maudhui ya unyanyasaji, chuki na yanahaibisha .

Amri hiyo maalumu inaainisha kuwa sheria ambayo italinda maudhui ya mitandao ya kijamii kama maudhui hayo hayajabilishwa kwa kuhaririwa na mtumiaji wa mtandao huo na kutaka sheria hiyo ibadilishwe au kuondolewa na wabunge kwa kifungu namba 230. Bwana Trump alisema mwanasheria mkuu William Barr ataanza mara moja kuandaa sheria ambayo itapigiwa kura.

Maamuzi hayo yanasema kuwa kuzuia maudhui ya mtu sio jambo la busara, pamoja na kujumuisha sababu ya kutochapisha maudhui hayo ambazo ziko tofauti na maelezo yaliyoandikwa katika sheria zilizopo kwenye huduma ya tovuti, amri hiyo mpya inataka lazima zilindwe.

Seneta wa Republican, Marco Rubio ni miongoni mwa watu wanaodai kuwa mitandao ya kijamii inachukua jukumu la mchapishaji hivyo wana haki ya kuongeza ukweli wa jambo katika baadhi ya machapisho.

"Sheria bado inalinda kampeni za mitandao ya kijamii kama Twitter kwa sababu wanajulikana kama jukwaa na sio wachapishaji," alisema bwana Rubio.

"Lakini kama wataamua sasa kufuata sheria za uhariri kama wachapishaji, basi watapaswa kutambuliwa kisheria kuwa wachapishaji."
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad