Mshukiwa wa Mauaji ya Watalaamu wa UN nchini Congo Akamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mmoja wa washukiwa wakuu katika mauaji ya watalaamu wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakichunguza makaburi ya halaiki katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amekamatwa baada ya msako wa miaka mitatu ya kiongozi huyo wa kundi la wapiganaji.

 Mkuu wa ofisi ya mwendesha mashitaka wa jeshi katika eneo hilo ameliambia shirika la habari la AFP kuwa Tresor Mputu Kankonde alikamatwa Jumamosi na anapelelezwa kwa sasa.

Luteni Kanali Jean-Blaise Bwamulundu Kuzola amesema Kankonde anatuhumiwa kwa makosa kadhaa yakiwemo mauaji ya watalaamu wa Umoja wa Mataifa.

Wachunguzi wa Umoja wa Mataifa Zaida Catalan na Michael Sharp, mwanamke wa Sweden mwenye asili ya Chile na mwanaume wa Kimarekani, waliuawa mnamo Machi 2017 katika mkoa wa Kasai ya Kati.

Walikuwa wanachunguza makaburi ya halaiki yaliyogundulika katika mgogoro kati ya vikosi vya usalama vya Congo na wapiganaji waasi wa kundi la Black Ant katika jimbo hilo la kati la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad