Kenya Yarekodi idadi Kubwa ya Wagonjwa Waliofariki na Virusi vya Corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa wa corona Kenya inakaribia 300 kulingana na takwimu zilizotolewa na serikali Jumanne.

Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alitangaza kwamba watu wengine 14 wamefariki kutokana na virusi hivyo katika kipindi cha saa 24 na hivyobasi kufanya idadi ya waliofariki kufikia sasa kuwa 299.

Aidha idadi ya wagonjwa waliothibitishwa kuwa na maradhi hayo imefikia 18,581 baada ya waziri wa Afya kutangaza wagonjwa wengine 606.

Kati ya wagonjwa hao wapya 583 ni raia wa Kenya huku 23 wakiwa raia wa kigeni , wanaume wakiwa 409 nao wanawake wakiwa 197.

Mgonjwa mwenye umri mdogo zaidi ni mtoto wa miezi minne huku mtu mwenye umri mkubwa zaidi akiwa mzee wa miaka 85.

Hatahivyo habari njema ni kwamba wagonjwa 75 wa corona wamepona maradhi hayo , na hivyobasi kufanya jumla ya waliopona nchini Kenya kufikia 7,908.

Mjini Nairobi eneo la Embakasi limetajwa kuwa na wagonjwa wengi na waziri huyo amewataka wakaazi kuchukua tahadhari.

Kagwe amewataka wale wanaofanya kazi kutoka nyumbani kujaribu kufanya kazi katika nyumba zao.

''Nimekuwa risasi, umekuwa risasi . Tunaweza kumuua mtu, Tumekuwa hatari'', alisema.

Amewataka wazazi kuwasisitizia watoto wao kuosha mikono , kupaka sanitizer na kuwajibika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad