Mwalimu Ajitia kitanzi Baada ya Mkewe Kumthibitishia Mimba si Yake, Amwachia Ujumbe Mzito

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Aliacha ujumbe mrefu kubainisha chanzo cha kujiua. Picha: Hisani




Caleb alikunywa sumu siku mbili baada ya kurudi kutoka Nairobi alikoenda kumtembelea mkewe

Mkewe aliomba talaka akidai kuwa mimba aliyobeba si yake

Aliacha ujumbe mrefu kubainisha chanzo cha kujiua

Huku janga la corona likizidi kuangamiza familia nyingi, katika familia nyingine, tofauti za kinyumbani zinazidi kuzua vifo.

Caleb, mwalimu katika kaunti ya Kakamega ameamua kujitia kitanzi baada ya kutofautiana na mkewe.

Katika kisa hicho kilichofanyika Alhamisi, Agosti 6, mwalimu huyo anadaiwa kumtembelea mkewe mjini Nairobi alikokuwa akifanya kazi

na kurudi Kakamega siku mbili baadaye.

Kulingana na Peter ambaye alikuwa rafiki yake wa karibu, Caleb alirudi kutona Nairobi baada ya kukosana na mkewe.

Nirbhaya convicts didn't bathe, skipped breakfast before hanging ...

Kulingana naye, mkewe huyo ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi saba alimuomba talaka akidai kuwa mtoto huyo hakuwa wake.

Inadaiwa kuwa suala hilo limuumiza Caleb na kumsukuma kurudi nyumbani haraka licha kuwa shule zimefungwa.

Inadaiwa kuwa mwalimu huyo alijitilia sumu kwenye glasi ya sharubati akainywa na kupatikana kwenye kochi akiwa amefariki.

Maafisa wa polisi waliofika eneo hilo walichukua karatasi ya ujumbe aliyomwandikia mkewe akimtakia maisha mema na marefu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad