Ghorofa yaporomoka na kusababisha vifo India

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Watu wasiopungua 10 wamefariki na watu 11 wamejeruhiwa kutokana na kuporomoka kwa jengo la gorofa nne nchini India.

Jengo la ghorofa nne limeanguka asubuhi katika wilaya ya Thane ya Mumbai, mji mkuu wa jimbo la Maharashtra.


Satya Pradhan, mkuu wa Kikosi cha Kitaifa cha Kukabiliana na Maafa, ameripoti kuwa watu wasiopungua 10 wamefariki na 11 wamejeruhiwa kutokana na kuanguka kwa jengo hilo.


Imeelezwa kuwa timu za utaftaji na uokoaji zimejaribu kuwafikia watu 20 hadi 25 ambao walikuwa wamekwama katika jengo hilo lililoporomoka.


Ni kawaida kuona majengo ya zamani yakiporomoka kwa sababu ya mvua za masika, haswa mnamo Juni na Septemba nchini India.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad