Kenya kushiriki katika jaribio la chanjo ya Oxford

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kenya itashiriki hatua za mwisho za jaribio ya kitabibu la chanjo ya virusi vya corona ambayo inatengenezwa na AstraZeneca na chuo kikuu cha Oxford.

Taifa hilo litakuwa la pili kutoka barani Afrika kushiriki katika jaribio ambalo lilisitishwa siku ya Jumatano, baada ya mshiriki mmoja kutoka Uingereza kupata madhara.


Tayari zaidi ya washiriki 1,000 kutoka Afrika Kusini wamehusishwa katika jaribio hilo kutoka Afrika Kusini.


Wafanyakazi wa afya wapatao 400 watashiriki katika jaribio ambalo litafanyika nchini Kenya katika pwani ya Mombasa na Kilifi.


Miji hiyo miwili ndio ilichaguliwa na serikali.


Chanjo inayotengenezwa na AstraZeneca-chuo kikuu cha Oxford ni miongoni mwa majaribio tisa mengine ambayo yamefanyika katika sehemu kubwa ya dunia.


Washiriki watapewa chanjo mara mbili katika wiki nne.


Na wataruhusiwa kuendelea na shughuli zao za kawaida. Kupata virusi hakutawafanya kutoka katika jaribio.


Jaribio litaangalia usalama wa chanjo, uwezo wa uzalishaji wa kinga na ufanisi wake.


Matokeo ya awali yatatolewa mnamo mwezi Novemba.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad