Rukhsa kununua na kunywa pombe Umoja wa Falme za Kiarabu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mamlaka katika mji mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Abu Dhabi imeondoa masharti ya kupata kibali cha kununua na kunywa pombe, baada ya mji jirani wa Dubai kuchukua hatua kama hiyo. 

Ulegezaji huo wa masharti katika miji hiyo unalenga kuikuza upya sekta ya utalii ambayo imeathiriwa vibaya na janga la virusi vya corona, na kujiandaa kuwapokea watalii kutoka Israel baada ya kuwekeana uhusiano wa kidiplomasia na nchi hiyo. 


Barua kutoka idara ya utamaduni ya mji wa Abu Dhabi imesema kuanzia sasa, wenyeji na wageni katika mji huo wataweza kununua pombe kutoka maduka yaliyoruhusiwa, bila kuhitaji vibali maalumu. 


Barua hiyo inasema pombe itakayonunuliwa sharti inywewe majumbani, au mahali palipoporuhusiwa kama vile kwenye baa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad