Ufaransa kuwapokea watoto 500 kutoka katika kisiwa cha Lesbo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



 Ufaransa yafahamisha kuwa pokea watoto wa wakimbizi  500 kutoka katika kisiwa  cha Lesbo Ugiriki.

Baada ya ajali ya moto iliotokea katika kambi ya wakimbizi katika kisiwa cha Lesbo, kisiwa ambacho ni milki ya Ugiriki, waziri wa Ufaransa anaehusika na masuala ya Ulaya Clement Beaune amefahamisha kuwa watoto 500 katika kisiwa hicho watappkelewa na kupewa hifadhi nchini Ufaransa.


Katika mahojiano yaliofanyika katika kituo cha redio cha RTL , Beaune ameendelea akifahamisha kwamba watu ambao wengine 150 wataorpdheshwa miongoni mwa wakimbizi ambao watapewa hifadhi nchini Ufaransa kutoka katika kisiwa hicho cha Lesbos Ugiriki.


Moto umekuwa ukitokea mara kwa mara katika kambi za wakimbizi kwa muda wa wiki mbili mfululizo.


Polisi na maafisa zimamoto wamekuwa wakilinda doria baada ya kuzima moto na kuwazuia wakimbizi kuleta ghasia. Wakimbizi waliokuwa wakitaka kuandamana hadi mjini Kati wamezuiliwa na jeshi la Polisi.


Kambi ya wakimbizi ya Lesbo imepokea wakimbizi zaidi ya 12 500.


Miongoni mwa wakimbizi hao, 35 wametengwa kutokana na maambukizi ya virusi vya corona .



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad