Joh Makini atambulisha lebo yake, amsaini Otuck William

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Rapper ameitambulisha lebo yake ya muziki iitwayo "Makini Records" pamoja na kumtambulisha msanii mpya Ptuck William ndani ya LEBO hiyo.

Akizungumza mbele wa waandishi wa habari , Joh Makini ambaye anawakilisha kundi la Weusi amesema amekuja na lebo hiyo ili kusaidia vipaji vipya viweze kujilikana kwenye kiwanda cha muziki wa Bongo.


Amesema kwa muda mrefu alikuwa anatamani kufanya hivyo lakini alikuwa anashindwa kutokana na mtaji wa kuwekeza ambapo kwa sasa amesema yupo tayari kuwasaidia wasanii wenye vipaji.


Joh amewataka mashabiki wake kuisapoti lebo hiyo ili kusaidia vipaji vya wasanii wa Bongo na kukuza muziki wa Bongo Fleva pamoja na muziki wa Hip Hop.


"Makini Records" tayari ina mwanamuziki mmoja aliyetambulishwa leo na ameshaachia kazi yake ya kwanza akiwa na Joh Makini, ngoma inaitwa "MbelekwaMbele".

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad