Wanajeshi wawili, wapiganaji 21 wauawa katika makabiliano DR Congo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Wanajeshi wawili na wapiganaji 21 wameuawa katika kipindi cha siku tatu za makabiliano katika mkoa wa Ituri, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 

Jeshi la serikali limesema lilizindua operesheni iliyoanza Ijumaa baada ya kutokea mashambulizi kadhaa kutoka kwa kundi la waasi wa CODECO.


 Luteni Jenerali Philemon Yav amesema wanajeshi wawili waliuawa na wengine wanne wakajeruhiwa katika eneo la Walendu Tatsi, mashariki mwa mji mkuu wa mkoa wa Ituri, Bunia. 


Amesema eneo hilo lipo chini ya udhibiti wa vikodi vya serikali baada ya makabiliano hayo yaliyoendelea hadi Jumapili, na kulazimisha idadi kubwa ya wakaazi kukimbilia usalama wao mwishoni mwa wiki. 


Waasi wa CODECO walikubali kusitisha mashambulizi dhidi ya wapinzani wao wa kikabila baada ya Rais Felix Tshisekedi kulituma Ituri kundi la wababe wa zamani wa kivita mwezi Agosti. Kundi hilo la kisiasa na kidini linatuhumiwa kwa mauaji ya mamia ya raia tangu Desemba 2017.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad