Unaambiwa Sarah Asepa na Kila Kitu Chake Kwa Harmonize

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





IMEVUJA! Aliyekuwa mpenzi wa staa wa Bongo Fleva, Rajabu Abdul ‘Harmonize’ Sarah ametimkia nchini kwao Italy na kuchukua kila kilichokuwa chake kwa zilipendwa wake huyo.


Chanzo chetu cha karibu kabisa na mrembo huyo, kimesema kuwa, Sarah aliamua kurudi kwao kwa sababu ya kuchoka na vituko vya Harmo tangu ilipojulikana kuwa ana mtoto wa nje na kuamua kumuweka hadharani.


“Unajua Sarah aliamua kunyoosha mkono juu na kusepa zake nchini kwao maana alishindwa kuvumilia kila kukicha visa hivyo aliona wazi hapendwi wala hathaminiwi,” alisema mtoa habari huyo.



Akiendelea kushusha ubuyu kama wote, mtoa habari huyo alisema, Sarah aliamua kuondoka kwa ajili ya kutotaka kukumbuka chochote walichokuwa wakishea na msanii huyo akiwa hapa nchini na kubadilisha mazingira mengine kabisa ili kupunguza machungu aliyokuwa nayo.


“Sarah ameondoka kwao lakini alikuwa na maumivu makali sana akaona bora aondoke labda anaweza kupunguza machungu aliyokuwepo nayo kutokana na Harmonize kumsaliti na kubadilisha kabisa hali ya hewa,” alisema mtu huyo ambaye ni wa karibu na Sarah.


Gazeti hili lilijaribu kumtafuta kwa njia ya meseji ya moja kwa moja kupitia mtandao wake wa Instagram lakini hata hivyo hakutoa ushirikiano wowote.


 DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL HAPA KUPATA HIZI HABARI KWENYE SIMU YAKO HATA BILA BUNDLE



Sarah na Harmo walioishi kwa miaka kadhaa bila kupata mtoto, walifunga ndoa ya kimila nchini Italy na kufanya tafrija nyingine hapa Bongo kabla ya kumwagana na kila mtu kushika hamsini zake.Kwa sasa Harmo ameonesha kujitosa mzimamzima kwenye penzi la mrembo kutoka Bongo Movies, Kajala Masanja

GPL
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad