Album ya Burna boy ya African giant imetajwa na Grammy kuwa ndio album bora Afrika (+ Video)

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Burna Boy, ambaye jina lake halisi ni Damini Ogulu, ambaye ameshiriki kwa mwaka wa pili ameshinda katika albamu yake ya Twice As Tall .


Tuzo ya Grammy ya 63 imefanyika mjini Los Angeles. Kwa kawaida huwa sherehe kubwa ya muziki huwa inafanyika kila mwaka lakini mwaka huu hali imekuwa tofauti kutokana na janga la corona.


Hakuna watazamaji, na watumbuizaji walikuwa wametengwa katika majukwaa matano, na wakiwa kwa umbali.


Burna Boy, mwenye miaka 29, amewashinda wengine wanne ikiwemo bendi ya Malian, Tinariwen.


Tuzo za Grammy zimeielezea albamu ya Twice As Tall kuwa muziki uliotengenezwa kwa kiwango cha juu cha kimataifa, ni fundisho kuwa pia kwa wegine na ndio maana imemfanya Burna Boy kuingia katika kiwango hicho cha kimataifa”.


“Aliendelea kusema kuwa kuwa albam hiyo imechanganya miondoko mbalimbali kama midundo ya pop, Afrobeat, dancehall, reggae na miondoko mingine mingi,” walieleza.


Albumu yake ilishirikisha wanamuziki wengi duniani wakiwemo Stormzy, Youssou Ndour, Naughty By Nature, na Chris Martin wa Coldplay, na vilevile Sean Combs akiwa muandaaji mkuu.


Video ambayo imemfanya Wizkid kushinda imeelezewa kuwa imezingatia mitindo na kusheherekea urembo wa mwanamke mweusi mahali popote duniani “.


Burna Boy amechaguliwa katika kipengele kilekile cha mwaka 2019 – kinachojulikana kama ‘Best World Music Album’ – lakini Angelique Kidjo aishinda katika tuzo za mwaka 2020.


Ingawa Kidjo aliamua kutoa ushindi wake kwa Burna Boy, alisema: “Burna Boy ni miongoni mwa wasanii wachanga ambao wanatoka Afrika ambao wanabadili mtazamo wa muziki wa Afrika.”


Mwanamuziki huyu aliyezaliwa Nigeria, Burna Boy alizindua albamu yake ya kwanza ya LIFE, mwaka 2013.


Na baadae alizindua albamu ya Redemption mwaka 2015 na Outside mwaka 2018 ambayo ilijumuisha ngoma iliyovuma kimataifa ya , Ye.


Lakini ilikuwa katika albamu yake ya mwaka 2019 ya African Giant ambapo Burna Boy alijulikana zaidi kimataifa na kupata tuzo yake ya kwanza ya Grammys.


Akiwa analinganishwa na mwanamuziki wa Nigeria Fela Ransome-Kuti na kupata umaarufu barani Afrika.


Wakati wa mgogoro wa ubaguzi Afrika Kusini mwaka 2019, alitishia kutoenda katika taifa hilo kama serikali ya nchi hiyo haitachukua hatua dhidi ya xenophobic.


Pia alijumuishwa katika maamndamano ya #EndSARS ya kupinga unyanyasaji wa polisi, alitoa wimbo wa wahanga ambao waliuawa katika maandamano hayo Oktoba 20,2020 katika geti la Lekki Toll Gate mjini Lagos.


Vilevile ameandika katika kurasa yake ya tweeter kuunga mkono waandamanaji wa Senegal ambao walijitokeza barabarani baada ya kiongozi wa upinzani Ousmane Sonkokukamatwa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad