Wanafunzi watekwa nyara Nigeria

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Takribani wanafunzi 150, hawajulikani walipo baada ya watu waliokuwa na silaha kuvamia shule ya bweni katika jimbo la kaduna nchini Nigeria na kutokomea nao kusikojulikana.



Jeshi la Polisi kwa kushirikiana  na wanajeshi wanawasaka wanafunzi hao. Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, shule hiyo ya upili ya Bethel Baptist ni ya 10 kushambuliwa kaskazini magharibi mwa Nigeria tangu Desemba, wakati mamlaka zikisema kuwa washambuliaji hudai fidia baada ya kuwateka nyara wanafunzi.

Ripoti zinasema kuwa idadi kubwa ya wazazi waliokuwa wakilia walikusanyika kwenye shule hiyo, wakitarajia kupata taarifa kuhusiana na waliko watoto wao. Ripoti za polisi zinasema kuwa washambuliaji waliingia saa za usiku na kuwazidi nguvu walinzi waliokuwepo huku wakitoroka na wanafunzi kuelekea kwenye msitu ulio karibu.

Hata hivyo taarifa zimeongeza kusema kuwa watu 26 akiwemo mwalimu mmoja wa kike wameokolewa. Mwanazilishi wa shule hiyo kasisi John Hayab ameiambia Reuters kwamba takriban watu 25 walibahatika kuponyoka wakati wanafunzi waliobaki walishikwa mateka na washambuliaji.

BY BAKARI WAZIRI

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad