Album ya Kanye West Kizungu Mkuti Huenda Isitoke Kisa Kumtoa Jay Z na Kumuingiza Rapper Dababy

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Album ya msanii @kanyewest ,DONDA haitatoka kama ilivyotarajiwa kuwa kuanzia siku ya jana ingekuwa premiered kwenye streaming sites,na Sababu kubwa ni meneja wa Dababy.



Hatujui ni kwanini Kanye West alimtoa Jay Z kwenye wimbo wa Jail ambao unapatikana kwenye albam ya DONDA na kumuweka @dababy lakini imeonekana kama gundu baada ya Meneja wa Dababy kukataa kupitisha verse ya Dababy kwenye wimbo huo na kufanya zoezi la album ya Donda kutoka kushindikana.

West amepost screenshots za chats kati yake na Meneja wake,BU pamoja na Dababy, Meneja wa Kanye west akieleza kuwa meneja wa Dababy amegoma kuipitisha verse ya msanii wake kwenye wimbo wa Jail na hivyo inabidi atolewe lakini West amegoma kumtoa Dababy kwenye huo wimbo maana ni mtu pekee aliyejitokeza hadharani na kuongea kuwa atampigia kura ya urais Kanye West.

Pia kwenye chats na Dababy,Kanye West amemwambia Dababy anaharibiwa kwenye game na watu wake wa karibu. Bado haijulikani suala hili litaisha lini japo watu wanadai uwenda Kanye West anategea Drake aachie Album yake kwanza ambayo inatarajiwa kutoka mwezi September.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad