Miquissone Kubaki Simba? Al Ahly Yampotezea

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





JARIBIO la Mabingwa wa Klabu Bingwa Barani Afrika, Al Ahly ya Misri 🇪🇬 kupata saini ya Luis Miquissone wa Simba Sc 🇲🇿 huenda likagonga mwamba licha ya kutoa Ofa kwa Klabu ya Simba SC 🇹🇿 ya zaidi ya bilioni 2 (dola za Marekani 900,000).

Mabingwa hao wa Kihistoria Barani Afrika kwa sasa wamekaa kimya kuhusu dili hilo huku ikielezwa kuwa nguvu yao kubwa sasa wameielekeza kupata saini ya winga wa Kimataifa wa Afrika Kusini, Percy Tau 🇿🇦.

 

Kocha wa Ahly Pitso Mosimane alitaka kunasa saini ya Miquissone ambaye ni raia wa Msumbiji kwa miaka minne baada ya Konde Boy huyo kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika michuano ya Mabingwa Afrika ambapo Miquissone aliifunga Ahly bao pekee walipokutana na Simba katika Dimba la Mkapa kwenye hatua ya makundi.

 

Taarifa kuhusu uhamisho wa Tau kutoka Brighton and Hove Albion ya Ligi Kuu ya Uingereza kwenda Al Ahly imeshika kasi nchini humo ambapo inaelezwa kuwa Mosimane amependa uchezaji wa Tau anayemfananisha na Lionel Messi.

 

Akizungumza na Goal.Com, Mosimane amesema; “Percy yupo imara kama Messi, ana vitu vingi vya kukupa kila wiki, acha tumpe nafasi,” amesema Mosimane.

 

Kwa upande wake, kuhusu Luis Miquissone 🇲🇿 kujiunga na Klabu ya Al Ahly 🇪🇬 Klabu ya Simba SC 🦁 imesema itatangaza hivi Karibuni kama amejiunga na Al Ahly 🇪🇬 au anabaki Simba SC.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad