Rais Samia awajia juu wanaosambaza sumu ya ukabila

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Rais Samia Suluhu Hassan ameonya viongozi wanaosambaza sumu ya ukabila baada ya kuwajibishwa wanapokuwa wameharibu kwenye majukumu yao huku akisisitiza yeye haangalii kabila kwenye kuteua mtu.
Ameyasema hayo leo Oktoba 11, 2021 Ikulu Chamwino Dodoma, wakati akiongea baada ya kuwaapisha viongozi wateule, Mhe. Sophia Edward Mjema, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Jaji Omar Othman Makungu, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mhe. Jaji Mustapha Siyani, kuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

''Watu wanafanya makosa ukiwashika ukiwawajibisha, nimewajibishwa kwa sababu ni wa kabila fulani, sina kabila mimi ukiniuliza kabila langu nani nitakwambia ni Mzanzibari. Hiyo sumu mnaipeleka sana na naomba isimame. Mwalimu Nyerere alitufundisha kufanya kazi bila kuangalia makabila,'' ameeleza Rais Samia Suluhu.

Aidha, amesisitiza kuwa, ''Mimi siangalii kabila, TAMISEMI kwa mfano Waziri ni Mtanga, Katibu Mkuu Mtanga na wengine, nikaletewa hapa mama umeweka wote watanga, nikauliza wana sifa? waacheni wafanye kazi wakikoroga nawatumbua, sipangi kwa makabila napanga kwa uwezo twende tukasukume maendeleo ya wananchi''.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad