Dalili za Omicron: Je mafua ni dalili ya virusi vya corona?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Aina mpya ya virusi vya corona vya Omicron vinaenea kwa kasi duniani kote. Je ni dalili gani watu wakipata wanapaswa kuchukua hatua?

Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema watu bado wanapaswa kuangalia dalili za kawaida za Covid:

aina mpya ya kikohozi kinachoendelea
homa/joto la juu
kupoteza au kubadilika kwa harufu au ladha
Mpaka sasa kwa mujibu wa baadhi ya data za Uingreza, dalili tano za virusi vya corona vya Omicron ni hizi:

Mafua mepesi
kichwa kuuma
uchovu
kupiga chafya
kikohozi
Kama unadhani kuwa una corona, ni muhimu kufanya vipimo.

Hata watu ambao hawajisikii vizuri wanaweza kuwaweka wengine katika hatari ya kuumwa .Lakini watafiti wanasema , kuwa na uviko 19 kunaweza kukufanya mtu ujisikie kama una mafua makali au baridi.

Je nikipata homa, ina maana nina virusi vya corona?

Kiwango cha juu cha joto cha 37.8C au kuendelea.

Homa kama hii inaweza kuja wakati mwili ukiwa unapambana na maambukizi na sio virusi vya corona tu.


Ni bora kutumia kipima joto-thermometer. Lakini ikiwa huna, angalia ikiwa wewe, au mtu ambaye una wasiwasi naye, anahisi joto kwa kuguswa kwenye kifua au mgongo.

Joto kali hali na baridi hivi, Ikiwa una homa, panga kufanya vipimo vya coronavirus.

Vipi kuhusu kikohozi?
Ikiwa una homa au mafua unaweza kuwa na kikohozi, pamoja na dalili nyingine.

Mafua kwa kawaida huja ghafla na wagonjwa mara nyingi watapata maumivu ya misuli, baridi, maumivu ya kichwa, uchovu, koo kuwasha na mafua kutiririka au kujaa puani, pamoja na kikohozi. Unaweza kujihisi vibaya zaidi kuliko baridi kali.


Baridi ina mtindo wa kuanza taratibu na haina maumivu makali, ingawa inakufanya usijisikie vizuri pia.

Pamoja na kifua, labda na kupiga chafya, maumivu ya koo na mafua .

Homa, maumivu ya mwili na kichwa kuumwa huwa ni maumivu yanayotokea mara chache.

Kikohozi cha virusi vya corona, huwa kinakufanya mtu ukohoe sana zaidi ya saa, saa tatu au zaidi ndani ya saa 24.

Kama huwa unakohoa kwa sababu unapata matibabu ya hali ya kiafya ya muda mrefu, basi kikohozi kitaongezeka na hali kuwa mbaya zaidi.

Unapaswa kupima virusi vya corona kama umeanza kukohoa kwa mfululizo.

Kupoteza au kubadilika kwa harufu au ladha kunamaanisha nini?
Hii ni dalili kuu za coronavirus na inamaanisha unapaswa kupimwa.

Bado inaweza kuwa una mafua tu, wakati wa baridi. Lakini unahitaji kuangalia, hata kama hujisikii vizuri, ili kuepuka hatari ya kueneza virusi.

Je, kupiga chafya kunamaanisha kuwa nina virusi vya corona?


Kupiga chafya sio dalili ya kawaida ya coronavirus. Matone ya kupiga chafya yanaweza kueneza maambukizi ingawa, hivyo ni muhimu kunawa mikono yako au kutumia tishu.

Ili kusaidia kuzuia kuenea kwa coronavirus na magonjwa mengine:

• Nawa mikono mara kwa mara

• Vaa barakoa katika mkusanyiko wa watu

• Jaribu kuwa mbali na wale ambao hawakai nyumbani kwako.

Vipi kuhusu mafua kutiririka au pua kuziba au maumivu ya kichwa?
Mamlaka ya afya yanasema kuwa na mafua au maumivu ya kichwa sio dalili za Covid.

Lakini utafiti unasema baadhi ya watu wanaopima na kukutwa na Covid wana dalili hizi.

Muongozo wa Marekani unaangazia dalili zifuatao kujua kama mtu ana uviko:

Homa
Kikohozi
Kupumua kwa shida
Kuhisi uchovu
Maumivu ya mwili na misuli
Maumivu ya kichwa
Kupoteza ladha au kubadilika kwa harufu
Koo kuwasha
Mafua
Kutapika
Kuharisha

Je kama sijisikii vizuri?

Watu walio na virusi vya corona wana dalili mbalimbali, kuanzia dalili kidogo hadi kali. Baadhi hawatakuwa nayo kabisa, lakini bado wanaweza kuambukiza.

Dalili zinaweza kuonekana hadi wiki mbili baada ya kuathiriwa na coronavirus, lakini kawaida karibu siku ya tano.

Kuhisi kukosa pumzi kunaweza kuwa ishara ya maambukizo makubwa zaidi ya coronavirus.

Ikiwa unapata shida ya kupumua, wasiliana na daktari wako mtandaoni au kupitia simu.

Ikiwa una wasiwasi sana juu ya upungufu wa pumzi ghafla, piga simu uletewe gari la wagonjwa.

Pata ushauri wa daktari kama :

Una wasiwasi kuhusu mtoto mwenye umri wa chini ya miaka mitano
Mtoto wako hajisikii vizuri ,tafuta ushauri wa daktari.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad