Mlinzi wa Shule Auawa, Wauwaji Wabeba Kichwa na Kutoweka Nacho

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Arusha. Mlinzi wa shule ya Winnings Spirit iliyopo eneo la Terati jijini Arusha, Issa Dinaiah (57) amekutwa ameuawa kwa kuchinjwa huku kichwa kikiwa hakipo.

Mwili wa mlinzi huyo umekutwa leo Jumatano Februari 2, 2022 asubuhi na wafanyakazi wa shule hiyo inayomilikiwa na Meya wa Jiji la Arusha, Maximilian Iranghe.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meya Iranghe amesema alipata taarifa za kifo cha mfanyakazi wake mmoja leo asubuhi na baada ya kufika eneo la tukio aliwakuta Polisi.

Iranghe amesema bado chanzo na waliofanya mauaji haya hawajajulikana.


"Naomba kuwasiliana na Polisi ambao ndio wanaendelea na uchunguzi wa tukio hili mimi nimepigiwa simu na wafanyakazi na nimekuta tayari polisi wapo hapa" amesema

Maofisa wa Jeshi la Polisi waliokuwa katika eneo la tukio wameeleza taarifa rasmi itatolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.

"Ni kweli tukio limetokea lakini msemaji ni Kamanda wa Polisi Mkoa atatoa taarifa rasmi "amesema mmoja wa maofisa wa Jeshi hilo ambaye alikuwa kwenye eneo la tukio.


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha, Mary Kupesha hakupatikana kutoa taarifa ya tukio hilo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad