Mastraika Simba Wachimbwa Mkwara Mzito

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KOCHA Msaidizi wa Simba, Seleman Matola, amefunguka kuwa benchi la ufundi la klabu hiyo halijaridhishwa na mwenendo wa ufungaji mabao ndani ya kikosi chao na tayari wamekaa na mastraika wa kikosi hicho kuangalia namna ya kumaliza tatizo hilo.

 

Simba msimu huu wamekuwa na changamoto kubwa kwenye safu ya ushambuliaji ya timu hiyo ambapo kabla ya mchezo wa jana walikuwa wamefanikiwa kufunga mabao 15 tu, katika michezo yao 14 ya mzunguko wa kwanza waliyokuwa wamecheza.

 

Kwenye Ligi Kuu Bara mpaka sasa kwa Simba ni Meddie Kagere pekee ambaye amefanikiwa kuandikisha mabao msimu huu akiwa tayari amefunga mabao matano, huku John Bocco na Chris Mugalu wao wakiendelea kuwa na ukame wa mabao.

 

Akizungumzia changamoto ya safu yao ya ushambuliaji msimu huu, kocha Matola alisema: “Kama benchi la ufundi tunakiri kuwa ni kweli tumekuwa na changamoto katika safu yetu ya ushambuliaji msimu huu, tatizo ambalo kama benchi la ufundi tunalifanyia kazi ili kuhakikisha linamalizika na tunafunga mabao.

 

“Tayari tumekaa na washambuliaji wetu na kuangalia wapi tunakosea ili kurekebisha, pia kuwaweka wazi kuwa hatuhitaji kuona hali hii inaendelea.”

JOEL THOMAS, Dar es Salaam

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad