Mwanamuziki Country Boy Afunguka Lebo yake ya Mziki Baada ya Kutoka Kwa Harmonize

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kwa sasa muziki wa Bongo fleva unakuwa kwa kasi sana kutokana na baadhi ya matukio ambayo tunaendelea kuyaona kunako muziki huu.

Miongoni mwa matukio yanayo tuonyesha ukuaji wa muziki huu ni kuchukuliwa kama ajira kwa vijana kwani muziki umekuwa msaada sana kwa vijana wengi Tanzania, na hilo analithibitisha rappa @countrywizzy_tz ambaye ameanzisha lebo yake mpya ya muziki kwaajili ya kuinua vipaji vingine ambavyo havijapata nafasi.

Country ameitangaza lebo hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameipa jina la @iam_music_co

Aidha, hatua hiyo inakuja ikiwa ni miezi mitatu imepita tangu aachane na Konde Music Worldwide.

"Kutokana na jitihada anazozionesha Rais wetu mpendwa, Mama yetu kipenzi MH SAMIA SULUHU HASSAN kuhakikisha Nchi yetu inasonga mbele mimi kama kijana sijataka kubaki nyuma Nimefungua kampuni iitwayo @iam_music_co ambayo itahusika katika kusaidia vijana mtaani ambao wengi wanatamani kutimiza ndoto zao lakini wanashindwa kutimiza kutokana na changamoto wanazokutana nazo.

Hivyo basi nakuja mbele yenu Watanzania na serikali kwa ujumla kuipokea KAMPUNI hii. Hatuna pesa nyingi lakini tunaamini katika kidogo tulichonacho kitatuvusha kutoka sehemu moja kwenda nyingne" - @countrywizzy_tz

✍️: @omaryramsey


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad