Urusi imembadilisha kamanda wake wa vita, afisa wa Magharibi athibitisha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Afisa wa magharibiamethibitisha kuwa Urusi imepanga upya uongozi wa operesheni zake za kivita katika Ukraine, na kumteua Jenerali mpya mwenye uzoefu wa mapambono ya kivita katika Syria kusimamia vita vya Ukraine.

Akizungumza mwandishi wa BBC Gordon Corera kwa sharti kwamba asitajwe jina lake, chanzo cha taarifa hii kilisema kuwa kamanda wa wilaya ya kijeshi ya kusini mwa Urusi, Jenerali Alexander Dvornikov, sasa ndiye anayeoongoza uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine.

“Kamanda huyo ana uzoefu mkubwa wa operesheni za Urusi nchini Syria. Kwahiyo tunamtarajiauongozi na udhibiti utaboreka ,” kilisema chanzo hicho.

Uteuzi mpya ulifanyika katika jaribio la kuimarisha uratibu baina ya vikosi mbali mbali , kwani makundi ya Urusi yamekuwa yakipangwa na kuongozwa na wakuu tofauti, alisema afisa.


 
Urusi hadi sasa inahangaika kufikia malengo yake ya kivita, ikishindwa kuichukua miji muhimu kama vile Kyiv kabla ya hatimaye kuelekeza macho yake katika jimbo la Donbas mashariki.

Afisa huyo alisema kuwa mbinu za Urusi zimekuwa zikiwafanya warudishwe nyuma na vikosi vyenye askari wachache wa Ukraine wanaopigana kwa akili zaidi na kwa kushitukiza-licha ya Urusi kufikiriwakuwaina kikosi "kikubwa" chenye bataliani 100 zenye wanajeshi wenye ujuzi.

“Bila kubadili mbinu zake ni vigumu sana kwa Urusi kufanikiwa kwa malengo yao waliyojiwekea wenyewe ," alisema afisa huyo.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad