Watu 8 Wafariki na Wengine 19 Kujeruhiwa kwa Ajali Mkoani Njombe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah amethibitisha kutokea kwa vifo vya watu 8 na 19 kujeruhiwa katika ajali ya gari aina ya Coaster T 287 CCY mali ya kanisa Katholiki Njombe iliyogongana na lori la makaa ya mawe.

Watu hao ni miongoni mwa Umoja wa vijana kanisa katoliki Jimbo la Njombe (UVIKANJO) ambao walikwenda kuwatembelea watoto yatima katika kituo cha Ibumila wilayani Njombe.


Orodha ya majina ya waliofariki kwenye ajali

Ajali ilitokea jana majira ya jioni katika eneo la Igima wilayani Wanging’ombe Barabara kuu (TANROADS) kuelekea mkoa wa Ruvuma.

Aidha amesema majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mji wa Njombe Kibena pamoja na hospitali ya rufaa ya mkoa huo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad