Hii Hapa Misumari Iliyotumika Kumsulubisha Yesu Msalabani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Pasaka ni siku kuu ambayo Wakristo karibu wote hufanya kila mwaka ukumbusho wa kufufuka kwake Yesu Kristo siku ya tatu baada ya kusulubiwa kufa na kuzikwa kwake. Mwaka huu maadhimisho yalifanywa Aprili 2 hadi 3.


Wataalam wanafikiri misumari hiyo ni mirefu ya kutosha kuwa imetundikwa mikono juu ya kusulubiwa, na inaweza kuwa imeinuliwa juu kuzuia mikono kuinuliwa.

Lakini je, ushawahi kujiuliza misumari iliyotumika kumsulubishaYesu msalabani iko wapi?

Utafiti wa punde umeonyesha kuwa kuna misumari ya nyakati za Roma iliyohifadhiwa kwenye sanduku lililoletwa katika Chuo Kikuu cha Tel Aviv ambayo inashukiwa huenda ni misumari miwili iliyodaiwa kupotea kutoka kwenye kaburi la kuhani mkuu wa Kiyahudi Kayafa, aliyemhukumu Yesu.

Misumari hiyo miwili iliyoshika kutu ambayo baadhi wamependekeza ndiyo iliyotumika kumsulubisha Yesu msalabani inaonekana kuwa iliyotumika nyakati za kale kusulubisha, kulingana na utafiti mpya, na hali hii imezua mjadala mpevu kuhusu zilikotoka misumari hiyo.

Uchambuzi wa punde uliofanywa unasema, misumari hiyo ndiyo iliyopotea kutoka kaburi la kuhani mkuu wa Kiyahudi anayedaiwa kumkabidhi Yesu kwa Waroma kusulubiwa. Vipande vya mbao na unga kutokana na mifupa vinaonyesha kuwa inawezekana vilitumika katika kumsulubisha Yesu.


Mtaalam wa jiolojia Aryeh Shimron, mwandishi mkuu wa utafiti uliochapishwa mnamo Julai, 2020 katika jarida la Ugunduzi wa Akiolojia (Archaeological Discovery), alisema uhusiano kati ya Kayafa na ushahidi wa hivi karibuni haukuthibitisha kabisa kuwa misumari hiyo ilitumika kumsulubisha Yesu huko Yerusalemu mnamo AD 33, lakini waliimarisha madai yaliyotolewa awali.

"Kwa kweli sitaki kusema kwamba misumari hii inatokana na kusulubiwa kwa Yesu wa Nazareti," Shimron aliiambia Live Science. "Lakini ni misumari iliyotumika wakati wa kusulubiwa? Ndio, kuna uwezekano mkubwa."

Misumari hiyo ilitoka wapi?
Sanduku hilo lenye mapambo ya kifahari, lililopambwa kwa nakshi za maua na kuandikwa kwa Kiaramu "Joseph mwana wa Kayafa," lilipatikana katika kaburi la karne ya kwanza huko Yerusalemu mnamo 1990. Misumari miwili ya chuma yenye kutu ilipatikana pia katika kaburi hilo, lakini baadaye ilipotea.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad