Mrembo Ashtuka Usiku wa Harusi Kutambua Mumewe Hana Miguu Yote

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Hadithi ya mapenzi kati ya Ndayisenga Jean De Dieu na mke wake Deborah 'Borah' Muteteri, ni ya kutia moyo.

Mrembo Ashtuka Kutambua Mumewe Hana Miguu Miezi Michache Baada ya Harusi
Ndayisenga amefichua kuwa alikatwa miguu yote akiwa na umri wa miaka saba. 

Wanandoa hao walikutana mwaka 2018 na kufunga pingu za maisha katika harusi ya kufana miezi michache iliyopita.

Apata mshtuko
Borah alikuwa anafikiria mpenzi wake ana miguu yote lakini alikuja kugundua kuwa miguu yake yote ilikatwa baada ya harusi yao.

Jamaa Aliyening'inia Kwenye Helikopta ya Waziri Munya Anaswa: "Atakabiliana na Sheria"
Akizungumza na Afrimax, Ndayisenga alizaliwa kawaida lakini alipokuwa na umri wa miaka saba, pamoja na familia yake walilazimika kukimbia nchini Congo sababu ya usalama.


 
Baada ya miaka kadhaa, waliamua kurejea nyumbani na wakiwa safarini, bomu ililipuka karibu nao na miguu yake iliathirika vibaya na kuingia katika coma kwa miezi miwili.

"Niliamka na kukuta mguu wangu mmoja umekatwa," alisema.

Kisha madaktari waliamua kukata mguu wake wa pili ambao haukuwa unafanya kazi.


Ndayisenga alifichua kuwa mama yake alikuwa naye wakati huo mgumu. Mama yake alipata mimba na alifariki baada ya kuzaa mtoto aliyefia tumboni.

"Katika kipindi cha mwaka mmoja, nilipoteza watu watatu wa familia yangu. Mdogo wangu, mama na ndugu mwingine," alisema.

Kisha alipewa magongo ambayo alijifunza kutumia kutembea nazo.

Baada ya kukamilisha shule ya upili, Ndayisenga, alishiriki kwenye mashindano ya kuimba kati ya watu walemavu na miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo ilikuwa Borah.


 
Niliachika Katika Ndoa Tatu Kisa Sikupata Mtoto, Ila Ndoa ya Nne Nimezaa Dume!
"Tulikutana kwenye mashindano. Tuliongea lakini naweza kuona alikuwa akitaka kujua ... aliendelea kuuliza ikiwa sikuwa na maumivu nikisimama kwa mrefu kwenye magongo," alikumbuka.

Wawili hao walibadilishana nambari za simu na kuanza kuzungumza. Baada ya kuzungumza kwa miezi mitano, Ndayisenga alianza kumpenda Borah lakini alikuwa anaogopa kumwambia kuwa hana miguu yote.

"Alijua nilikuwa na miguu yote miwili na akafikiria ni jeraha la kawaida kwa sababu sikuwahi kumuonyesha miguu yangu," alisema

Baada ya kuzungumza kwa miezi mitano, Ndayisenga alimpenda Borah lakini alikuwa anahofia kumjuza kuwa hana miguu.

"Alijua nilikuwa na miguu yote miwili na akafikiria ni jeraha la kawaida kwa sababu sikuwahi kumuonyesha miguu yangu. Nilidhani ikiwa angejua kuwa sina miguu," angeniacha.


Harusi
Wapenzi hao waliamua kutoshiriki ngono wakichumbiana hadi watakapoingia katika ndoa na walitimiza ahadi zao.

Usiku wa harusi yao, Ndayisenga aliamua kumwambia Borah kuhusu ulemavu wake na alishtuka sana.

"Baada ya kunionyesha ni nani, ilinipa sababu milioni za kumpenda zaidi. Ilinipa nguvu za juu. Niligundua lazima nifanye zaidi ili yeye awe na furaha na kusahau historia yake. Nilisema ingawa hana miguu, hiyo haitazuia kumpenda," alisema.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad