"Diamond alinifukuza Wasafi kisa kushiriki video ya Harmonize" - mcheza densi Sholey

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mcheza densi wa Rayvanny, Sholey
Mcheza densi rasmi wa msanii Rayvanny Sholey amefunguka kilichosababisha yeye kufukuzwa katika miradi ya video za msanii Diamond Platnumz.

Akizungumza na mwanablogu wa YouTube, Sholey ambaye amekuwa akionekana kwenye video za wasanii wengi tu ndani na nje ya WCB Wasafi tangu mwanzo kama vixen alisema alishtukia ghafla ametemwa kutoka kikosi cha vixens wa Diamond Platnumz.


Sholey alisema kwamba tangu mwanzo amekuwa akicheza kwenye video za ngoma za wasanii Diamond Platnumz, Harmonize, Rayvanny na hata Lavalava lakini hatua ya kutemwa kutoka kuonekana kwenye video za mhusika wa pale – Diamond Platnumz bila kujuzwa sababu ilihujumu nafsi yake sana mpaka kujihisi kukosa amani kuendelea kuwepo pale.

Alisema kwamba alihisi kutemwa kwake kulikuja pindi tu baada ya kuonekana kwenye wimbo wa Harmonize, Ushamba, wimbo ambao msanii huyo aliutoa muda mrefu tu baada ya kuondoka Wasafi kwa shari.

Ila alisisitiza kwamba yeye kucheza kweney wimbo wa Harmonize hakukuwa tatizo kwa sababu hakuwa na mkataba ndani ya Wasafi ulikuwa unamwekea mipaka ya wasanii wa kufanya kazi nao na wale wa kutofanya kazi nao.


“Kutoka tu popote nilijipata nimetolewa kwenye kazi za mhusika wa lile eneo. Mimi nilihisi ni kwa sababu ya kutokea kwenye wimbo wa Harmonize ‘Ushamba’ mimi ni mcheza densi tambua, nafanya kazi popote. Diamond hakuniambia kwamba Sholey naomba usicheze kwa mtu yeyote,” alisema vixen huyo.

Sholey alielezea kwamba wapambe wa Diamond ndio walimwambia atoke kwenye mradi wa wimbo wa Diamond ambao alikuwa ashiriki kucheza kwa kile walimtajia kwamba hana msimamo na ana tamaa ya kuonekana kote kote mpaka kwenye upande wa mahasidi wa Diamond – kwa maana ya kuonekana kwenye video ya Harmonize.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad