Wema Sepetu Atamba Kuwazidi Wanawake Bongo Kwa Followers Instagram

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Supastaa Wema Sepetu ambaye ni Miss Tanzania mwaka 2006 ni habari nyingine, nyota huyo ambaye ana miaka zaidi 16 kwenye gemu ni miongoni mwa mastaa wa kike nchini waliyodumu kwenye kiwanda cha burudani kwa muda mrefu akiwa bado anaendelea kusumbua.

Good news kwa mashabiki wa @wemasepetu ni kwamba amefanikiwa kufikisha followers Milioni 10 kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram na kuwa mwanamke wa kwanza Tanzania kufanya hivyo.

Aidha, Wema amebainisha kwamba hataki kushindanishwa na yeyote yule kwani naye hajawahi kushindana na mtu. Ameeleza kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kuongoza kuwa na followers wengi kwa wanawake nchini.

"Nabaki kuwa wa kike wa kwanza Tanzania kufikisha 10M, basi naombeni kuanzia sasa, msinishindanishe na mtu jamani. Atakaefuata na kunizidi isiwe battle basi wapenzi wangu. Tumefikisha 10M bila nguvu yoyote, nitumie tu nafasi hii kusema ASANTENI na NAWAPENDA. ❤️💚❤️." - @wemasepetu

Fahamu, anayemfuata Wema ama kumkaribia ni mwanamitindo Hamisa Mobetto ambaye ana followers Milioni 9.9, kisha Shilole mwenye followers Milioni 9.4


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad