AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
KIWANGO bora kinachoendelea kuoneshwa na Yanga katika mashindano mbalimbali msimu huu, kimemuibua Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said ambaye ameweka wazi kuwa, wana matumaini makubwa ya kufanya vizuri na kuandika historia mpya katika Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu.
Yanga ambao leo Jumapili wanatarajiwa kushuka kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar, kuvaana na Geita Gold katika mchezo wa wa Ligi Kuu Bara, ndio wawakilishi pekee wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika wakiwa Kundi D.
Yanga wamekuwa kwenye kiwango bora msimu huu ambapo baadhi ya mastaa wa kikosi hicho akiwemo Fiston Mayele na Kennedy Musonda, wakionesha uwezo mkubwa katika mashindano tofauti.
Kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi, Mayele na Musonda wamechangia mabao matatu mpaka sasa.
Akizungumza na Spoti Xtra, Injinia Hersi alisema: “Tunafurahia ubora wa kikosi chetu na matokeo ambayo tumeendelea kuyapata, hii inaonesha ni kwa kiasi gani kama timu tumeamua kufanya makubwa msimu huu.
“Kwenye Kombe la Shirikisho Afrika tuna nafasi nzuri ya kucheza robo fainali ikiwa tutaibuka na ushindi dhidi ya US Monastir, tunaamini kuwa kwa ubora wa kikosi tulionao tunaweza kuandika rekodi katika mashindano ya Afrika msimu huu.”
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK