Rais Samia aongeza tiketi 5,000 kuiona Stars

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais Samia Suluhu Hassan ameongeza tiketi alizotoa kwa ajili ya mashabiki kufikia 7,000 kutoka 2,000 za awali.

Tiketi hizo zitakazotolewa kwa mashabiki ni sehemu ya hamasa ya Rais kuelekea mchezo wa marudiano kati ya Tanzania na Uganda utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Machi 28 mwaka huu.

Tiketi hizo ni sehemu ya tiketi 20,000 ambazo Serikali inatoa kwa mashabiki bure kuingia uwanjani kuishangilia timu ya Taifa.

Katika mchezo huo, na ijayo, Rais pia ameahidi kutoa TZS milioni 10 kwa kila goli ambalo Taifa Stars itafunga.

Stars inahitaji alama tatu, ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2023, ambazo zitafanyika nchini Ivory Coast Januari 2024.

Endapo itafuzu, Stars itakuwa imefikia hatua hiyo kwa mara ya tatu, ambapo mara ya mwisho ilifuzu mwaka 2019.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad