Serikali kumlipa mshahara Kocha wa Taifa Stars

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Waziri wa Utamaduni, Sana na Michezo Mhe, Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuendeleza mchezo wa Soka nchini itamlipa mshahara mwalimu wa Timu ya Taifa (Taifa Stars),


Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa hafla ya  kumtambulisha Kocha huyo, Machi 07, 2023 Mtumba jijini Dodoma, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali inaamini Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limejiridhisha kuwa ni Kocha Bora atakayekuza soka la Tanzania.


" Ukitazama wasifu wa Kocha Adel utabaini uzoefu mkubwa alionao sio tuu katika kufundisha soka uwanjani, bali pia katika kuandaa Wataalamu wengine wa Soka, hivyo tumtumie vizuri ili asaidie timu yetu kufanya vizuri ndani na nje ya nchi"


Ameongeza kuwa, Serikali inaendelea kuangalia uwezekano wa kupata wataalamu katika michezo mingine ambapo ameeleza kuwa Wizara inaendelea kuimarisha Wataalamu wa michezo kupitia Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichoko wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.


Kwa upande wake Kocha Amrouche ameahidi kuwanoa  wachezaji vyema ili kuiweka juu zaidi  Tanzania katika ulimwengu wa Soka , huku akisisitiza ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali katika kufanikisha kazi

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad