Mwanaume Akamatwa Akifanya Biashara ya Ngono Mwanza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limemkamata kijana mmoja aliyekuwa akijiita jina la kike la Asmat Abdalah na kuacha jina lake halali la Isma Abdalah kwa lengo la kuwalaghai wanaume kuwa yeye ni mwanamke amekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza.

Akizungumza na vyombo vya habari, leo Mei 12, 2023 Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema kijana huyo alikamatwa katika eneo la Bar maarufu ya Villa Park iliyopo Kirumba Ilemela Mkoani humo akiwa amepanga mstari akisubiri wanaume kwa lengo la kumnunua ili kuingiliwa kinyume na maumbile.

"Huyu kijana alikuwa akijiita jina la Asmat lakini yeye jina lake halisi ni Isma, huyu tumembaini wakati tunataka kumuweka katika sero ya wanawake, kabla ya kuwaweka sero lazima ukaguzi ufanyike na baada ya kumkagua tulibaini ana jinsia ya kiume,” amesema Kamanda Mutafungwa.

Aidha Kamanda Mutafungwa ameeleza kuwa kijana huyo atafikishwa mahakamani kwa kosa la kuruhusu kuingiliwa kinyume na maumbile.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad