Eng. Hersi Afunguka "Leo Tutawapiga Mabao Waarabu Kama Tulivyowafanyia Tunisia"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KUELEKEA mchezo wa fainal ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger utakaopigwa leo Jumamosi nchini Algeria, Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said ametamba kuwa licha ya kipigo cha mabao 2-1 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza wana matumaini makubwa ya kupindua meza kama walivyofanya dhidi ya Club Africain ya Tunisia.

Yanga ambao waliondoka nchini juzi Alhamisi ambapo leo Jumamosi wanatarajia kushuka kwenye Uwanja wa 5 July 1962 kuvaana na USM Alger, katika mchezo wa fainali ya mkondo wa pili unaotarajiwa kupigwa majira ya saa 4 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Kikosi hicho kinaingia katika mchezo wa leo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo wa fainali ya kwanza kwa kipigo cha mabao 2-1, mchezo uliopigwa Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Hersi alisema: “Tupo tayari kwa ajili ya mchezo huu muhimu, kama timu tunajua wapi tulipoteleza kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza na tayari tumefanya marekebisho na tunaamini huu utakuwa mchezo tofauti.

“Kuna baadhi ya watu wanadhani mchezo umeisha kwa kuwa tulipoteza mabao 2-1 nyumbani, lakini niwahakikishie kuwa tuna nafasi ya kuwashangaza watu kwa kupindua meza hapa Algeria kama ambavyo tulifanya dhidi ya Club Africain kule Tunisia.”

Stori na Joel Thomas
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad