Dada wa Wema Sepetu Ashitakiwa Marekani Kwa Utakatishaji Mabilioni ya Fedha

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

Dada wa Wema Sepetu Ashitakiwa Marekani Kwa Utakatishaji Mabilioni ya Fedha

Dada wa dMiss Tanzania 2006, Wema Sepetu, Sunna Sepetu (37) ametiwa mbaroni mjini Worcester, Massachusetts nchini Marekani baada ya kukutwa na hatia ya kula njama ya utakatishaji fedha zilizotokana na utapeli.

Mshtakiwa mwenzake, Nafise Quaye, (47) raia wa Nigeria ambaye pia anaishi Worcester, Massachusetts pia alitiwa hatiani kwa shtaka kama hilo kufuatia kesi ya siku nane katika mahakama ya shirikisho. Wawili hao wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 jela.

Uamuzi huo ulitangazwa na Wakili wa Marekani Jane Young, ambaye alisisitiza dhamira ya Idara ya Sheria ya kuwashtaki wale wanaowezesha ulaghai wa mtandao unaolenga watu walio hatarini.

“Uamuzi huu unasisitiza uzito ambao Idara ya Haki ya Marekani inatazama ulaghai wa mtandao unaolenga watu walio hatarini,” alisema Wakili wa Marekani Jane Young.

Kati ya 2013 na 2019, Sepetu na Quaye walidaiwa kupokea takriban $3.2 milioni (zaidi ya Sh8 bilioni) kutoka kwa mwathiriwa wa ulaghai huko Texas.

Fedha hizo zilihamishiwa kwenye akaunti za benki zilizoanzishwa na washtakiwa kwa majina ya makampuni mbalimbali ya kandarasi.
_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad