Familia ya Gcaba Yakanusha Kuhusika na Mauaji ya Rapa AKA

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

 

Familia ya Gcaba Yakanusha Kuhusika na Mauaji ya Rapa AKA

Familia yenye ushawishi mkubwa nchini Afrika Kusini Gcaba imekanusha uvumi kuwa mmoja wa wanachama wake alihusika katika mauaji ya rapa maarufu AKA. jina halisi la Kiernan Forbes, na rafiki yake wa karibu, Tibz Motsoane, waliuawa kwa kupigwa risasi nje ya mgahawa mmoja huko Durban Februari mwaka jana.


Jumatano iliyopita, waendesha mashtaka katika kesi inayowakabili wanaoshukiwa kuwa wauaji wa rapa huyo walimhusisha Sydney Mfundo Gcaba, mmoja wa familia ya Gcaba, katika mauaji ya rapa huyo.


Taarifa iliyowasilishwa mahakamani na afisa wa uchunguzi ilidai kuwa kampuni moja ya Bw Gcaba ilituma zaidi ya rand 800,000 ($42,000; £33,000) kwenye akaunti ya benki ya Mziwethemba Harvey Gwabeni, mmoja wa washukiwa wanaoshtakiwa kwa mauaji ya rapa huyo.


Ripoti kwamba malipo hayo yalifanywa siku moja baada ya mauaji ya AKA yalizidisha shaka kwamba huenda Bw Gcaba aliwalipa washukiwa wa mauaji hayo.


Mwendesha mashtaka pia alidai kuwa hakuna uthibitisho kwamba Bw Gwabeni alitoa huduma badala ya pesa hizo.


Lakini katika taarifa iliyotolewa Jumapili, familia ya Gcaba ilisema kwamba malipo hayo ni sehemu ya shughuli kadhaa kati ya Bw Gcaba na Bw Gwabeni, ambazo "zilikuwa kwa madhumuni ya biashara".


"Shughuli hizi nyingi kwa muda mrefu zinaweza kuthibitishwa kupitia rekodi za benki na hazikuwa za kipekee wala kutengwa," taarifa ya familia ilisema.


Familia hiyo iliongeza kuwa "ilikuwa na wasiwasi" kwamba mamlaka haijamtaka Bw Gcaba kueleza upande wake wa hadithi, na kwamba alikuwa tayari kusafisha jina lake.

_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad