Kendrick Lamar Mshindi Beef Yake na Mwanamuziki Drake

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa




Rapa Kendrick Lamar amenufaika na bifu yake na Drake, baada kushika namba moja kupitia chati kubwa za muziki duniani (Billboard Hot 100) kupitia wimbo wake wa “Not like Us” ambao ni Diss track kwenda kwa Drizzy.

Kupitia chati mpya ya Billboard Hot 100 Kendrick Lamar amejitengenezea historia mpya kwenye maisha yake ya muziki mara baada ya kuwa rapa pekee kwa mwaka 2024 aliyeweza kuweka ngoma 2 kushika namba moja kwenye chati hizo.

Mbali na hiyo amejiongezea orodha ya ngoma alizowahi kushiriki na kufanikiwa kushika namba moja kwenye chati hizo “Bad blood” aliyoshirikishwa na Taylor Swift uliotoka mwaka 2014, “Humble” mwaka 2017 pamoja na “Like That” unaomilikiwa na Future & Metro Boomin ulioachiwa mwaka 2024.

Hasimu wake Drake ndie rapa anayeongoza kushika namba moja kupitia chati hizo na amefanikiwa kushika namba moja katika ngoma alizoshiriki mara 14, ila imekuwa tofauti kwenye bifu yake na Kendrick Lamar amefanikiwa kushika namba saba kupitia wimbo wake wa “Family matters”
_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad