Simba Yatangaza Vita Kubwa Dhidi ya Azam FC

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

 

Simba Yatangaza Vita Kubwa Dhidi ya Azam FC

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa vita ya ubingwa sasa imekufa na rasmi vita inahamia kwenye kusaka nafasi ya pili dhidi ya Azam FC ili kucheza Ligi ya Mabingwa Msimu ujao.


Ahmed amesema hayo baada ya Yanga kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa mara ya 30 jana kwa kumfunga Mtibwa Sugar na kufikisha alama 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote.


“Tunashindana na timu ambazo zinakaribia kukata roho, Imani yetu ya kushika nafasi ya pili ni kubwa mno, ni sisi wenyewe kama Simba kurekebisha mapungufu yetu na kuboresha mazuri yetu tukashike nafasi ya pili.


“Vita zote zimekufa rasmi sasa vita yetu ni moja tu dhidi ya Azam kuhakikisha tunashinda mechi zetu na kushika nafasoi ya pili ili tucheze Ligi ya Mabingwa msimu ujao.


“Mchezo dhidi ya Kagera ilikuwa tumalize mapema kipindi cha kwanza lakini makosa madogo yalitugharimu tukatoa sare,” amesema Ahmed.

_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad