Zitto Kabwe Aitikia Wito wa Polisi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Zitto Kabwe Aitikia Wito wa Polisi
Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Doroth Semu amefika katika kitengo cha uhalifu wa makosa ya kifedha kilichopo Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Semu amefuatana na Katibu wa Kamati ya Ulinzi ya chama hicho, Mohamed Babu.

Viongozi hao pamoja na Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo, Yeremia Maganja wanatakiwa kufika katika kitengo hicho wakiwakilisha wajumbe wote wa Kamati Kuu ambao walitakiwa kuripoti leo.

Wakati viongozi hao wakiwasili hapo, Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe ameripoti Kituo cha Polisi Chang'ombe jijini Dar es Salaam ambako anatuhumiwa kwa uchochezi.

Baada ya kuripoti kituoni hapo, Zitto ametakiwa kurejea tena Ijumaa Novemba 17,2017.

“Nimeambiwa nirudi wiki ijao siku ya Ijumaa Novemba 17," amesema Zitto.

Kiongozi huyo ameelekea Kamata ambako anatakiwa kuripoti katika kitengo cha uhalifu wa makosa ya kifedha.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tena kwesho kutwa anaitwa Kituoni Mtwara.

    ReplyDelete

Top Post Ad