AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Yanga imefanikiwa kutinga katika hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kufanikiwa kuiondoa Wolaitta Dicha ya Ethiopia kwa jumla ya mabao 2-1.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Julio alisema linapokuja suala la kitaifa utani uwekwe pembeni na watu wote waungane na kuwa kitu kimoja kwa lengo la kuusogeza mbele mpira wetu.
“Nimefurahi Yanga kuingia hatua ya makundi kwani imesaidia Tanzania kuendelea kusomeka katika ramani ya mpira, ukiangalia leo hii Tanzania tunasomeka kupitia wachezaji Samatta (Mbwana) na Msuva (Simon).
“Kwa hiyo kama wamepata nafasi hiyo ni fahari kwa Tanzania japokuwa kuna utani wao wa Simba na Yanga kwenye mitandao unaendelea ambao unaweza kuwa na faida au hasara kwa pande zote mbili. Kwa sasa tuangalie utaifa kwani itatusaidia.
“Utani wetu ubaki utani na linapokuja suala la kitaifa watu wote tuungane tuwe kitu kimoja na kuiunga mkono Yanga japokuwa kuna watu wengi wa Simba hawakupendezewa na hatua hiyo kufuatia utani wao wa Simba na Yanga,” alisema Juli
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Hicho kitu julio angekizumza wakati SIMBA inacheza na Almasry sio leo.
ReplyDelete