AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema watekaji hao walikuwa wakimuuliza Mo Dewji kuhusiana na masuala ya fedha, naye akawaambia wampigie baba yake mzazi ingawa hawakufanya hivyo.
"Mo amesema watekaji hao walitaka fedha. Hata hivyo yeye aliwasisitiza kumpigia baba yake kwa kuwa yeye alikuwa nao pale," alisema.
Mo amerejea nyumba ikiwa ni siku ya tisa baada ya kutekwa na watu wasiojulikana Alhamis Oktoba 11 katika Hoteli ya Colessium iliyopo Masaki jijini Dar es salaam.
Ameungana na familia yake akiwa salama baada ya kupatikana usiku wa kuamkia leo kutokana na watekaji hao kumuachia wakitumia gari lilelile walilotumia kumteka.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK