AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Diamond alifunguka mambo mengi ikiwemo Zari kum-cheat kwenye mahusiano, kuhusiana na kutoa sapoti kwa wanaye, na mambo mengine yaliyokuwa yanawahusu walipokuwa kwenye mahusiano.
Majibu ya Zari yalitoka rasmi wakati Diamond akiwa live kwenye mahojiano ambayo yalikuwa yanaruka moja kwa moja kwenye mitandao ya kijamii, radio na televisheni.
Zari alituma video tatu kwenye akaunti yake ya Instagram zilizokuwa na maelezo yanayosomeka: “Sasa yale magoti mpaka Sauzi yalikuwa ya nini? Kule kuomba msamaha kwote kwa radio kwa nini? Kwani umekuwa comedian sasa? Usinichafulie maisha bro. Yameisha zamani kubali tu. Kiki zimekuwa ngumu mjini. Niheshimu tafadhali nakulelea watoto tena vizuri”.
Video ya kwanza Zari amelalamikia kushushiwa heshima na kusema kwamba Diamond anajitetea kwa kumsingizia kwamba alikuwa na mahusiano mengine wakati bado wakiwa pamoja.
2.”Usibonyeze button kwa sababu nikianza kuongea juu yako, utajificha”. Zari amefunguka kuhusiana na Support ya watoto anayoipata kwa Diamond, kuhusu kuwa na mawasiliano na watoto, Pia Zari amesema kuwa hajaelewa inakuwaje Diamond anapata moyo wa kujiamini kwenda kwenye media na kumdhihaki kwa kumsingizia kuhusiana na mahusiano ambayo hajashiriki.
Lingine alilofunguka Zari ni kuhusiana na mahusiano yake na Mr P wa Psquare na Personal Trainer wake, amesema kwamba, “Kama nyie watu mtaamini maneno yanayotoka mdomoni mwa mwanaume kama huyu, yule yule aliyekataa damu yake, anakimbilia kwenye radio, anafanya ziara, kama kweli mnamuamini mtu huyu basi nyie wote ni wapumbavu kama yeye. Naomba tuheshimiane, kaa mahali ulipo, mi nipo nilipo, Mimi na watoto tupo vizuri bila wewe. Naomba tuheshimiane”
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Yaani huyu dada ukimsikiliza alivyojibu utafurahi, amejibu kwa hekma na busara sana, tofauti na tabia za wanawake wakati ukiwachokoza. Sio vizuri kumuongelea mtu vibaya baada ya mahusiano yenu kuvunjika. Alivyojibu zari inaonesha wazi kujiheshimu na kumuheshimu mzazi mwenzake.
ReplyDeleteEnter your comment...yetu masikio tu part 2 inakuja mengi tutayasikia
ReplyDelete