T.I Ajibu Tuhuma za Kuwadhalilisha Wanawake Kingono 'Mimi na Mke Wangu Hatujawahi Husika na Biashara ya Ngono Wala Kubaka"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


 T.I. na mkewe wamevunja ukimya, wameibuka na kukanusha tuhuma za unyanyasaji wa kingono zilizotolewa na wanawake zaidi ya 25 wiki hii.


Rapa huyo ametumia njia ya video kuzungumzia suala hilo, amesema tuhuma hizo ni uongo na hazina ukweli wowote. "Kwa nguvu zote na hekima tunakanusha tuhuma hizi za kipuuzi zilizotolewa na watu wasiofahamika." ilisomeka caption kwenye video hiyo yenye dakika 8.


T.I. aliendelea kusema kwamba ilikuwa ngumu kuweza kukaa kimya kufuatia tuhuma hizi ambazo pia zinamchafua na mkewe Tiny Harris. Anaamini amechafuliwa (defamed) kwa sababu wanaomtuhumu hawajafungua shauri lolote mahakamani.

-

"Hatujawahi kumlazimisha mtu yeyote, hatujawahi kumuhusisha mtu yeyote kwenye masuala ya kingono, hatujawahi kumteka mtu yeyote pasina ridhaa yake. Hatujawahi kusafirisha chochote, yani kinachohusu biashara ya ngono." alisema T.I. na kukanusha pia tuhuma za kubaka, "Sijawahi kumbaka mtu yeyote, kamwe sijawahi kumbaka yeyote."

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad