Panya Road Afunguka Jinsi Wanavyofanya Uhalifu "Tunaiba Alafu Tunagawana"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limesema limeendelea kuisimamia operesheni maalum kali na msako wa mtaa kwa mtaa dhidi ya Vijana wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu maarufu Panya Road na mpaka May 6,2022  limewakamata Wahalifu 31 kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya uporaji baada ya kuvunja nyumba, kujeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya nyumbani.

Miongoni mwa waliokamatwa ni Yunus Jafar Kwalo (20) ambaye amesimulia jinsi wanavyofanya uhalifu.

"Matukio yetu ya kiuhalifu huwa tunafanya usiku, tunakutania Mtaa wa Msumbiji (Chanika) Mnara wa Voda, suala la kuiba huwa halipangwi Watu wanatoka na kuingia kila nyumba baada ya hapo kuna Mtu anachukua vile vitu na kuondoka navyo na kisha vinauzwa mnagawana hela"

"Anayetutuma ni Rafiki yetu yeye ni mkubwa kuliko sisi, tukiuza mali tunagawana kinachopatikana, Elfu 50 hadi Laki 1, Wazazi wangu hawafahamu ninachokifanya, kilichonishawishi kufanya uhalifu ni marafiki, mapanga alikuja nayo Rafiki yangu yalikuwa kwenye mabegi"

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad