Ahmed Ali Ashindwa Kuvumulia Kinachoendelea Simba...Atoa Tamko

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

Ahmed Ali Ashindwa Kuvumulia Kinachoendelea Simba...Atoa Tamko


Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amewataka mashabiki wa timu hiyo kuwa watulivu wakati huu inaonekana kuwepo kwa sintofahamu

Ahmed amesema hata bahari kuna wakati huchafuka lakini baada ya machafuko kupita, utulivu hurejea

"Bahari hata ikichafuka vipi lakini kuna wakati inatulia, Wavuvi na Wasafiri wanaendelea na shughuli zao kama kawaida."

"Wavuvi na Wasafiri wenzangu msiwe na hofu punde bahari itakaa sawa na maisha yetu yataendelea kama kawaida," alisema Ahmed

Kumekuwa na sintofahamu baada ya taarifa ya kujiuzulu kwa baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi huku Wajumbe wengine kugoma kujiuzulu na kuibua kinachoonekana kama mgogoro baina ya Wajumbe wa Bodi upande wa Wanachama na Mwekezaji Mohammed Dewji

_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad